Web Templates
Country Profile  
Attractions  
Home  
 
 
 

  Sign Up
News and Events Visa Guestbook Trade Tourism Investment
 
Tanzania
  ABOUT MISSION
  ABOUT TANZANIA
  TANZANIA ATTRACTIONS
  BUSINESS
  EMBASSIES 
  VISA
  NEWS & EVENTS
  GALLERY
  GUEST BOOK
  REGISTRATION
  VISA FORM
  PASSPORT
 

MKUTANO WA WATANZANIA - WAJASIRIAMALI UINGEREZA

 

Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Taasisi ya Kusaidia Mazingira ya Uwekezaji Afrika (Investment Climate Facility for Africa), Bw. Omar Issa amekutana na Wajasiriamali wa Kitanzania waishio Uingereza na kuwapa changamoto ya kuanzisha biashara nyumbani.

Katika Mkutano uliofanyika jana katika jengo la Ubalozi wa Tanzania, London Uingereza (Tanzania House), Bw. Issa aliainisha fursa nyingi za biashara zilizopo Tanzania baada ya Serikali kufungua milango zaidi ya uwekezaji na kupatikana kwa wawekezaji wakubwa wa Kimataifa.

Akifafanua zaidi mtaalam huyo alisema hivi sasa takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania inahitaji zaidi biashara za uwezo wa kati (medium enterprises) ili kuziba pengo kubwa kati ya wafanyabiashara wakubwa na wadogo. Alisema ili kuendelea zaidi kiuchumi, makampuni makubwa yanahitaji sana makampuni ya kati kwa ajili ya kutengeneza mali ghafi, kuzalisha nguvu kazi na kutoa ushauri wa kitaaluma.

Katika Mkutano huo ulihudhuriwa na watanzania zaidi ya 30, Bw. Issa aliwashauri wajasiriamali hao kubuni miradi mbalimbali itakayowawezesha kupata mikopo kwenye benki za Tanzania ili kuweza kuanzisha biashara huko nyumbani. Aliwapa changamoto kuangalia fursa za biashara za huduma na ushauri wa kitaaluma.

Alisema benki nyingi hivi sasa nchini Tanzania zinawatafuta wenye miradi ya uhakika ili kuwakopesha mitaji ya kufanya biashara nchini humo. Alisema kwa elimu, upeo na uzoefu waliokuwa nao, wajasiriamali hao wanaweza kuanzisha miradi mizuri itakayowezesha kuinua uchumi wa Tanzania.

Kwa mafanikio zaidi, Bw. Issa amewashauri wajasiriamali hao kujiunga katika vikundi ili kuweza kujumuisha utaalam na mitaji ya msingi ya kuanzisha miradi hiyo. Alisema biashara nzuri inahitaji utafiti wa soko, udhibiti na shauku ya maendeleo zaidi.

Katika maswali yao kwa mtoa mada, wajasiriamali hao walipenda kufahamu mipango zaidi ya Serikali kuondoa urasimu. Bw. Issa aliwaambia kwamba wakati Serikali inaendelea na hatua mbalimbali kurekebisha mazingira ya uwekezaji na biashara nchini Tanzania, ni vyema Watanzania hao pia kutimiza wajibu wao badala ya kukaa tu kusubiri Serikali kufanya kila kitu. Alifafanua kwamba Watanzania walioko nje ya nchi wana uwezo mkubwa sana wa kubadilisha mazingira ya uwekezaji kama watarudi nyumbani na kuingiza utamaduni mpya wa kikazi.

Awali akimkaribisha mtoa mada, Balozi Mwanaidi Sinare Maajar alisema kwamba Ubalozi hivi sasa unafanya jitihada za kuwaunganisha wajasiriamali wa Kitanzania wa ngazi zote walioko Uingereza ili kuwashirikisha kikamilifu na Baraza la Biashara la Tanzania (Tanzania Business Council).

Bw. Issa yupo London kwa ajili ya Mkutano wa Uwekezaji wa Africa (Africa Business Forum 2008) ulioandaliwa na Commonwealth Business Forum.  

Picha zaid za Mkutano huo zinapatikana hapa>>>>

 

President Kikwete meets with Commonwealth leaders in London 

10 Commonwealth leaders gathered in London on June 9 and 10 2008 to discuss the reform of international institutions such as the World Bank and the International Monetary Fund.

President Jakaya Mrisho Kikwete was among 12 Commonwealth leaders who attended a mini-summit. The Heads of Government Meeting on Reforms of International Institutions ended up with the leaders expressing intention to redefine the purposes and governance of Bretton Woods institutions. They pledged to work towards a Commonwealth consensus and wider international support for an international conference to achieve these goals.
Accelerating World Bank, IMF and UN reforms and their effective implementation was a key intention outlined by the leaders.

Others who attended the meeting chaired by Prime Minister Gordon Brown of the United Kingdom include President Bharrat Jagdeo (Guyana), President Maumoon Gayoom (Maldives), Prime Minister Dr Navinchandra Ramgoolam (Mauritius), President Mahinda Rajapaksa (Sri Lanka), Prime Minister Dr Feleti Sevele (Tonga), Prime Minister Patrick Manning (Trinidad and Tobago), President Yoweri Museveni (Uganda), Deputy Prime Minister Najib Tun Razak (Malaysia) and Vice-President Alhaji Aliu Mahama (Ghana).

Read more on http://www.thecommonwealth.org
 

 


 

 

News and Events Visa Guestbook Trade Tourism Investment Registration

© Copyright 2003-2007 Tanzania High Commission