| |
|
PASIPOTI ZA TANZANIA
Kufuatia maulizo mengi kuhusu utoaji wa
Pasipoti Mpya, ufuatao ni utaratibu wa kushughulikia zoezi
hili kwa Watanzania waishio Uingereza na Ireland.
Pasi zote zilizotolewa awali zenye kurasa
36 zimesitishwa kutumika tena kwa safari; kuanzia tarehe 30
September 2005. Kwa mantiki hiyo basi, pasi hizo sio Pasi
halali za safari.
Kwa Mtanzania yeyote mwenye makazi yake
hapa Uingereza ama Ireland; iwapo atapata safari ya dharura,
kabla ya kupatiwa Pasi mpya ya kusafiria ama kubadili Pasi
ya Kusafiria ya zamani, anatakiwa awasiliane na Afisa
Uhamiaji, Ubalozini London; ili kuandaa taratibu za kupatiwa
Pasi ya Dharura ya Kusafiria.
|
A.
UPATIKANAJI WA FOMU ZA PASI MPYA
Mwombaji anaweza kuja
Ubalozini ili kununua fomu au atume GB Sterling Pounds (£)
5.00,- (malipo ya fomu kwa rejista). Aidha, alete bahasha
yenye anuani yake iliyobandikwa stampu za rejista ili
apelekewe fomu. (Aweke pound 5.00 malipo ya fomu)
-
Wale watakaopenda kuja Ubalozini kununua fomu na
kurudisha fomu wazingatie utaratibu ulioelezwa hapa
chini kifungu B.
-
Kila fomu ina namba maalum (Unique Identity No.),
haiwezi kutumika kwa watu wawili. Mwombaji asithubutu
kutoa nakala (photocopy) ili itumike kwa mwombaji
mwingine.
-
Watanzania wanaokwenda nyumbani
siku za karibuni wanashauriwa na wanaruhusiwa kuomba
pasipoti mpya wakati wakiwa nyumbani katika ofisi za
uhamiaji Tanzania. Kufanya hivyo kutawaharakishia
kupata pasipoti hizo na kupunguza gharama za
kufuatilia ubalozini London.
-
Inatahadharishwa kuwa fomu za uombaji pasipoti
zilizokosewa au kufutwafutwa hazitakubalika itabidi
mwombaji anunue fomu nyingine. Ni vema kabla ya kujaza
fomu mwombaji atoe nakala (photocopy) ya fomu aijaze
kwanza kila kipengele ili baadaye anakili katika fomu
aliyopelekewa kuepuka makosa ya kufutwafutwa na
kununua fomu nyingine.
B.
UTARATIBU WA KUOMBA PASI
Malipo yakipokelewa,
mwombaji atapewa fomu au atapelekewa fomu husika ambayo
ataijaza BILA kuweka sahihi yake katika
sehemu ya sahihi, ukurasa wa kwanza na wa pili.
- Jaza ukurasa wa kwanza na wapili tu, yaani kifungu cha
1 - 5 tu. Pia jaza karatasi ya alama za vidole.
Tunasisitiza kuwa uje na fomu zimejazwa tayari. Sehemu
ya anwani ni yoyote unayoitaka wewe.
- Sehemu yenye habari za wazazi wa mwombaji zijazwe
kikamilifu. Sehemu za mahali pa kuzaliwa zijazwe kama
fomu inavyoeleza. Kama hufahamu vizuri uliza wenzako
kabla ya kuja. Kujaza sehemu ya mama mzazi, jaza majina
yake ya ukoo na sio majina yake ya kuolewa.
Mwombaji anatakiwa kuleta:
- Fomu yake, na iliyokwishajazwa tayari.
Kama huelewi uliza wenzako.
- picha tano (5) za pasipoti zenye
`background' ya rangi ya ` blue' au rangi ya maji ya
bahari. Picha hizo lazima ziwe za hivi karibuni na zenye
kuonyesha masikio yote mawili.
- Nakala au kivuli cha Pasi ya zamani
(photocopy) kurasa tatu (3) za kwanza,ukurasa wenye
kibali cha makaazi (visa) na ukurasa wa mwisho wenye DN
au IF.
- Muda wako wa kuchukuliwa alama za
vidole ni kati ya saa 4 hadi saa 6.30 alasiri. Baada ya
hapo hakuna huduma hiyo.
Wakati wa kujaza fomu `Section 2' tarehe, mwezi na mwaka wa
kuzaliwa wazazi ni LAZIMA.
*FOMU IJAZWE KWA
HERUFI KUBWA!
-
Kama kuna sababu ya kubadilisha jina lazima hati
husika za sababu ya kubadili jina ziletwe - k.m. cheti
cha ndoa, au hati maalum za kubadili majina (deed
poll).
-
Kama pasipoti imepotea LAZIMA ripoti ya polisi na
`affidavit' (hati ya kiapo) mbele ya mwanasheria
zitumwe pamoja na fomu na maelezo yako bunafsi ya
ulikozaliwa, kuishi, ilikotolewa pasi na lini, na
imepoteaje.
-
Acha au usijaze kipengele cha sita (6) katika fomu kwa
kuzingatia Maelezo Muhimu kwenye kipengele cha pili
(2) - waliotajwa hawapatikani nje ya Tanzania.
C.
ALAMA ZA VIDOLE
Katika
utoaji wa pasipoti mpya lazima mwombaji achukuliwe alama za
vidole (`finger prints') na kuweka sahihi kwa mkono wake
mwenyewe mbele ya afisa mhusika.
Kufanyiwa
alama za vidole, Mwombaji anatakiwa kuomba kupewa siku ya
ahadi (Appointment).Hivyo Mwombaji anatakiwa kuwasiliana na
Ubalozi kwa kupiga simu, ama kutuma barua pepesi. Fomu
zinaweza kuchukuliwa siku yoyote, na Mwombaji haitaji ahadi
(Appointment) ili kupata fomu.
- Mwombaji anatakiwa aje UBALOZINI ili kutia sahihi
fomu na kuchukuliwa alama za vidole.
Mwombaji atatakiwa alipe jumla ya GB Sterlin Pounds
(£ ) 45 [5 kwa ajili ya fomu na 40 kwa ajili ya
pasipoti].- malipo ya pasipoti mpya.
- Maombi yatashughulikiwa na kupelekwa haraka Makao
Makuu ya Uhamiaji Dar es Salaam.
- Pasi mpya zitatolewa Makao Makuu ya Uhamiaji, Dar es
Salaam na kuletwa Ubalozini.
- Pasipoti ya zamani itabidi ifutwe hivyo mawasiliano
na Ubalozi ni muhimu.
- Utaratibu mzima wa kushughulikia unatazamiwa
kuchukua wiki sita (6) au zaidi.
- gharama GB Sterlin Pounds (£ ) 45,- yaani £ 5 za
fomu na £ 40,- pasipoti.
TAHADHARI:
Pasipoti mpya zitatolewa
kubadilisha zile ambazo zilizotolewa kihalali na zenye
kumbukumbu za utoaji kwa raia wa Tanzania. Siyo kwa wale
wenye uraia wa nchi nyingine walio na pasipoti mbili.
Kisheria nchi yetu hairuhusu `dual citizenship'; kufanya
hivyo ni kinyume cha sheria. Akigundulika
mwombaji mwenye uraia wa Tanzania na nchi nyingine
atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Aidha pasi za Tanzania
hazitolewi kwa watu wenye sifa za ukimbizi. Kama kwa
udanganyifu au bahati mbaya watajwa hapo juu walipata pasi
zetu wanamiliki kinyume cha sheria na tutatangaza kuzifuta.
- Watoto watapewa pasipoti zao kwa
kuzingatia utaratibu ulioelezwa.
- Watoto wa umri usiozidi miaka mitano
hawatachukuliwa alama za vidole vyote.
D.
WALIOPOTEZA PASI
Kwa waliopoteza Pasi, LAZIMA kuwasilisha
pamoja na maombi yako vitu vifuatavyo:
- Ripoti ya polisi kuthibitisha
kupotea/kuibiwa kwa Pasi ya Mwombaji
- Mwombaje atoe maelezo binafsi kwa
maandishi wakieleza yafuatayo:
- Taarifa za Pasi iliyopotea,
- Mazingira ya Pasi ilivyopotea/kuibiwa,
- Mahali Pasi ilikotolewa
- Tarehe na mwaka Pasi ilipotolewa, Namba ya
Pasi na DN.
- Tangazo la gazeti kuhusu kupotea pasi.
- Ni juu ya mwombaji kutafuta taarifa hizo, asije
kuuliza ubalozini atakavyopata vitu hivyo.
- Kwa mtu asiye na uthibitishi wowote ni vigumu kweu
kumpa huduma. ukishindwa kabisa wasiliana na wazazi
nao wapeleke uthibitisho huo uhamiaji makao makuu.
Taratibu za kawaida za kuomba Pasi zitafuata
baada ya Mwombaji kukamilisha maelekezo ya hapo juu.
E.
KUJUMUISHA WATOTO KATIKA PASI YA MZAZI
Kwa utaratibu wa pasi
mpya, watoto wadogo au walio chini ya umri wa miaka 18
hawataingizwa katika pasi za wazazi. Kila mtoto itabidi
aombewe pasi yake mwenyewe.
F.
HATI YA DHARURA [ Fomu za
Hati Ya Dharura ]
- Hii pasi itatolewa kwa misingi ya dharura tu, na
taratibu za kuomba zitafuata masharti yale yale ya pasi
ya Tanzania.
- Mtu aliye na pasi isiyokwisha muda hatopewa hati ya
dharura. Labda kwa maelezo maalumu yatakayomridhisha
afisa wa pasi.
- Ukipoteza pasi na unataka ya dharura, itakubidi
kufuata masharti yaleyale ya kupoteza pasi kama
ilivyoelezwa hapo awali.
- Pasi hii hupatikana kwa malipo ya paundi 20.00
na katika kipindi cha ndani ya wiki moja inakuwa tayari.
- ulete picha 3 rangi yoyote
- Utajaza fomu na hainunuliwi, utaipata katika
website yetu
- Lete kivuli cha Pasi yako
- Waweza kutuma maombi kwa posta lakini mahitaji
yake yakamilike.
|
|
|
|